Jumuia ya nchi za Kiarabu
imeamua kuuomba Umoja wa Mataifa uisaidie kuunda ujumbe wa amani wa
pamoja, kuutuma Syria, ili kumaliza ghasia nchini humo.
Uamuzi huo ulifikiwa katika mkutano wa jumuia hiyo, unaofanywa Cairo.
Piya mawaziri walikubali kusitisha uhusiano wa kibalozi na Syria, na kuanza mazungumzo na upinzani wa Syria.
Mkuu wa Jumuia ya Nchi za Kiarabu, Nabil
El-Araby, aliuambia mkutano kwamba wakati umefika kuchukua hatua thabiti
kumaliza adhabu za watu wa Syria.
0 maoni:
Post a Comment