16 Februari, 2012 - Saa 04:47 GMT
Shirika la kutetea haki za
binadamu, Amnesty International linasema visa vya mateso, mauaji na watu
kuzuiliwa bila kufunguliwa mashataka vimekithiri nchini Libya.
Shirika hilo linasema ukiukaji huo unatekelezwa na makundi ya wapiganji waliojihami ambao walimng'oa Muammar Gaddafi madarakani.
Walioathirika zaidi ni watu wanaohofiwa kuwa wafuasi wa Gaddafi, waafrika weusi na wahamiaji walioko Libya.
Kufuatia visa hivyo makundi ya watu waliolengwa sana na visa hivyo wamehama makaazi yao.
Shirika la Amnesty international linasema serikali mpya ya Libya imeshindwa kuwachukulia hatua watu wanaotekeleza vitendo hivyo.
Kuanzia mwezi uliopita BBC imekuwa ikikusanya
ushaidi wa mateso yanaoendelea miji ya Misrata, Gharyan na kusini mwa
mji mkuu Tripoli.
Ijumaa hii, sherehe zitafanyika kote nchini
Libya kuadhimisha mwaka mmoja tangu mapinduzi yaanze ambayo yalitarajiwa
kuleta mabadiliko.
Kuna wasiwasi mkubwa sasa kuwa watu waliosaidiwa
na NATO kuupindua utawala wa zamani, sasa wanahatarisha siku za baadaye
za nchi hii.
0 maoni:
Post a Comment