WELCOME TO THE REPUTABLE BLOG IN TOWN WITH FANTASTIC NEWS,GOSSIP,TALENTS,FASHION,MOVIE STAY ON THIS WEBSITE
RSS

Raia wa Libya 'auawa kizuizini

 18 Januari, 2012 - Saa 16:16 GMT


Daktari amtibu mpiganaji wa Gharyan
BBC imeona ushahidi wa mtu mmoja kuteswa na kuuliwa akiwa kizuizini, baada ya mapigano baina ya wapiganaji wapinzani nchini Libya mwishoni mwa juma.
Watu kutoka familia ya Izzedine al-Ghool wamesema alishutumiwa kwa kuunga mkono uongozi wa marehemu Kanali Muammar Gaddafi.
Waliokuwa makamanda waasi walisema wameanzisha harakati mpya za kuwanyang'anya silaha waliomtii Gaddafi waliopo maeneo ya Gharyan, kilomita 80 kusini mwa Tripoli.
Takriban watu tisa waliuawa katika mapigano yaliyotokea wiki iliyopita, maafisa walisema.
Waziri mkuu wa serikali ya mpito Abdurrahim al-Keib na waziri wa ulinzi Osama al-Juweili walitembelea eneo hilo katika jitihada za kusimamisha mapigano.

'Mshtuko wa umeme'

Mapigano hayo yanasemekana kuibuka baada ya wapiganaji wa Gharyan walipowakamata watu wanaoshukiwa kuwa na uhusiano na uongozi wa marehemu Gaddafi kwenye mji wa Assabia, takriban kilomita 16 kusini- magharibi mwa nchi hiyo.
Imeripotiwa wapiganaji wa Assabia walikataa kuwakabidhi washukiwa, na kuchochea mapigano ambapo roketi na bunduki nzito za rashasha zilirushwa.
Mwandishi wa BBC Gabriel Gatehouse, mjini Tripoli, aliripoti familia ya Bw Ghool ilisema alikuwa kamanda wa kikosi maalum cha wapiganaji kwenye eneo lake la asili Assabia, na alitiwa kizuizini siku ya Ijumaa baada ya mapigano kuanza.
Lakini wamekanusha kuwa bado alikuwa na utii kwa uongozi uliopita.
Kwa sasa mwili wake umewekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti kwenye mji mkuu.
BBC imeona alama kwenye miguu na makalio yake inayoashiria kuwa aliteswa sana.
Mwandishi wetu alisema hili ni suala nyeti kwa uongozi wa mpito.
Ofisa wa jeshi katika chumba hicho cha kuhifadhi maiti aliikatalia BBC ruhusa ya kumhoji daktari aliyefanya uchunguzi wa maiti hiyo.
Lakini muuguzi aliyekuwepo wakati mwili huo ulipofanyiwa uchunguzi alisema Bw Ghool aliadhibiwa kwa mshtuko wa umeme na kupigwa kupita kiasi.
Siku ya Jumapili, kamanda wa jeshi la Gharyan alisema watu wake waliteka idadi kadhaa ya wafungwa, ambapo mpaka sasa wameachiwa

  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

0 maoni: