Kundi la kwanza la wakimbizi wa Sudan Kusini ambao walikuwa wamekwama katika kambi za Sudan waanza kuelekea nyumbani. Kuna zaidi ya wasudan Kusini 15,000 ambao wamekwama Sudan baada ya kupewa makataa ya kuhama Khartoum. Mwezi uliopita wakimbizi hao walitajwa kama tishio kwa usalama wa Sudan na waliamriwa waondoke na warudi kwao Sudan Kusini. Agizo hilo la kuhama ni baada ya Sudan Kusini kupata uhuru hivyo basi raia wake waliokuwa wakiishi Sudan kuambiwa kuwa wamepoteza uraia wao. Shughuli hiyo yakuanza kuwasafirisha raia hao wa Sudan Kusini kunafuatia hatua ya Mkuu wa shirika la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa Navi Pillay kuishutumu Sudan kwa kuishambulia Sudan Kusini kwa mabomu licha ya kuagizwa na umoja wamatifa kumaliza uhasama kati yao. Siku ya jumatano Sudan kusini iliilaumu jirani yake Sudan kwa kushambulia maeneo yake kwa mabomu lakini Sudan ikajibu kwa kusema kuwa inahaki yakujibu mashambulizi yeyote. Mipango ya kuwasafirisha wasudan kusini kutoka maeneo kama vile Kosti yalio white Nile yanafanywa na shirika la kusaidia wakimbizi la IOM. |
Wasudan Kusini kurudishwa toka Khartoum
Posted by
RAMADHANI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 maoni:
Post a Comment