Wakazi wa wilaya ya muheza jijini Tanga wamelalamika wakitaka barabara ya Muheza pangani iwe katika kiwango cha lami kwani barabara hiyo imekuwa ikaharibu vyombo vya usafiri vitumiavyo barabara hiyo kwani barabara hiyo hadi sasa ipo katika kiwango cha vumbi na mashimo shimo hayo yamesemwa na wakazi wa wilaya hiyo walipokuwa wakifanya mahojiano na blog hii muheza mjini (Copec) na kutoa lawama sana kwa serikari kwani wawajui nini hatima ya barabara hiyo imekuwa gumzo sana kipindi cha mvua hivyo kusababisha vyombo vya usafiri kukwama kutokana na mvua zinazo endelea mkoani humo hivyo wameiomba serikari kupitia mbunge wa wilaya hiyo aliyefahamika kwa jina la Mheshimiwa Mtangi licha ya kipindi cha nyuma kuwa na matatizo ya tuhuma za rushwa katika kura za maoni wananchi hao wamelalamika nao wangependa waangaliwe kwa jicho la tatu kwa kuwa wamemchagua awapelekee kero zao sehemu husuka blog hii ilijaribu kumtafuta mheshimiwa lakini juhudi ziligonga mwamba kwa kuwa namba ya mheshimiwa mbunge ilikuwa haipatikani lakini bado ipokatika jitihada za kumtafuta kuongea naye Mheshimiwa juu ya mipango hiyo ya marekebisho ya barabara hiyo |
WAKAZI WA MUHEZA WATAKA MAREKEBISHO YA BARABARA YA MUHEZA PANGANI IWE KATIKA KIWANGO CHA LAMI
Posted by
RAMADHANI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 maoni:
Post a Comment