WELCOME TO THE REPUTABLE BLOG IN TOWN WITH FANTASTIC NEWS,GOSSIP,TALENTS,FASHION,MOVIE STAY ON THIS WEBSITE
RSS

MFUMUKO WA BEII TANZANIA

Mfumuko wa bei umepungua’  

Ibrahim Yamola
OFISI ya Takwimu ya Taifa (NBS), imesema mfumuko wa bei umepungua kutoka asilimia 19.0 Machi mwaka huu na  kufikia asilimia 18.7 Aprili mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa Jijini Dar es Salaam jana na  Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu,  Dk Albina  Chuwa alisema, katika kipindi kati ya Aprili mwaka jana na Aprili mwaka huu kumekuwa na mwenendo mzuri wa bei kwa huduma mbalimbali.

 “Kupungua kwa mfumuko wa bei Aprili mwaka huu kuna maanisha kuwa kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwezi uliopita imepungua ikilinganishwa na kasi ya upandaji Machi mwaka huu” alisema Dk Chuwa na kuongeza:

Mfumuko wa bei umekuwa na mwenendo wa kupanda kutoka asilimia 8.6 Aprili 2011 na kufikia asilimia 19.8 Desemba 2011 ambapo kuanzia Januari mwaka huu mwenendo wa mfumuko wa bei ulianza kushuka kutoka asilimia 19.7 hadi kufikia asilimia 18.7 Aprili mwaka huu.

Dk Chuwa alisema, mfumuko wa bei wa vyakula na vinywaji baridi umepungua hadi kufikia asilimia 25.3 Aprili mwaka huu kutoka asilimia 25.7 Machi mwaka huu.

“Kasi ya ongezeko la bei kwa bidhaa zisizo za vyakula imepungua hadi asilimia 11.2 mwezi uliopita  kama ilivyokuwa Machi mwaka huu” alisema Dk Chuwa.

Dk Chuwa alifafanua kuwa mfumuko wa bei ambao haujumuishi vyakula na nishati kwa Aprili mwaka huu umeongezeka  hadi asilimia 9.0 kutoka asilimia 8.8 Machi  mwaka huu.
“Kwa upande mwingine mfumuko wa bei wa nishati umepungua hadi asilimia 24.9 Aprili mwaka huu kutoka asilimia 29.4 Machi mwaka huu” alisema Dk Chuwa

Dk Chuwa  alisema , baadhi ya vyakula vinavyochangia kuongezeka kwa bei ni pamoja na mchele kwa asilimia 3.0,mahindi asilimia 1.6,unga wa mahindi asilimia 0.5,vitafunwa asilimia 7.3,unga wa mihogo asilimia 6.7,mayai kwa asilimia 2.1,siagi asilimia 2.9,machungwa asilimia 6.8,ndizi mbivu asilimia 4.8.

“Bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa bei ni pamoja na mavazi asilimia 0.9,gesi asilimia 3.9,mafuta ya taa asilimia 2.3,mkaa asilimia 5.3,Petroli asilimia 3.9 na begi za mikononi kwa asilimia 5.6” alisema Dk Chuwa.

  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

0 maoni: