WELCOME TO THE REPUTABLE BLOG IN TOWN WITH FANTASTIC NEWS,GOSSIP,TALENTS,FASHION,MOVIE STAY ON THIS WEBSITE
RSS


Bwana Wade, mwenye umri wa miaka 85, alisema kuonesha hasira kwa fujo hakutaleta tija yoyote.
Alitokeza kwenye televisheni huku ghasia zinatapakaa katika miji kadha ya Senegal.
Katika mji mkuu, Dakar, vizuizi viliwekwa, magari yalipinduliwa na maduka kadha yalichomwa moto.
Wakuu wanasema askari polisi mmoja aliuwawa.
Mpinzani maarufu, mwimbaji Youssou N'Dour, ameonya kuwa hukumu ya mahakama ya katiba haitakubalika.
Mahakama hayo yalitupilia mbali ombi la Bwana N'Dour kutaka kugombea urais katika uchaguzi wa mwezi ujao.


  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

0 maoni: