WELCOME TO THE REPUTABLE BLOG IN TOWN WITH FANTASTIC NEWS,GOSSIP,TALENTS,FASHION,MOVIE STAY ON THIS WEBSITE
RSS

200 wajeruhiwa wakitafuta kazi Tunisia

Mmoja wa waliojeruhiwa wakitafuta ajira huko Tunisia
Zaidi ya watu mia mbili walijeruhiwa huko Tunisia Jumatano katika siku ya pili ya maandamano jijini Siliana kilomita mia moja Ishirini kutoka katika jiji kuu la Tunis.
Waandamanaji hao walikuwa wakimtaka gavana wa eneo hilo kujiuzulu, kutaka msaada wa kiuchumi na vile vile kushinikiza watu kumi na wanne waliokamatwa katika ghasia za Aprili kuachiliwa.
Maafisa wa usalama walitumia gesi ya kutoa machozi na risasi za mipira kuwatwanya watu waliokuwa wanataka ajira. Pia kulikuwa na ripoti za watu kutibiwa baada ya kupata majeraha ya risasi.
Vyama vya wafanyakazi vimeitisha maandamano zaidi baadaye leo.
Tunisia ndiyo ilikuwa kitovu cha mapinduzi ya kiraia katika nchi za Kiarabu ambapo wananchi walimng'oa mamlakani rais wao wa muda mrefu Januari mwaka 2011.

  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

0 maoni: