4 Agosti, 2012 - Saa 12:46 GMT
Waziri wa Mashauri ya Nchi za
Nje wa Marekani, Hillary Clinton, amekutana na viongozi wa Kenya katika
sehemu ya mwisho ya safari yake ya Afrika.
Bi Clinton alisema mazungumzo yake yalihusu maswala kadha pamoja na uchaguzi wa mwaka ujao nchini Kenya, na hali katika nchi ya jirani, yaani Somalia, ambako wanajeshi wa Kenya wanapigana na kundi la wapiganaji wa Kiislamu, Al Shabaab. Bibi Clinton anaarifiwa kuiambia Kenya kuwa Marekani iko tayari kuisaidia Kenya kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka ujao, na Marekani inataraji uchaguzi huo utafanywa kwa salama. Bibi Clinton piya alitarajiwa kukutana na wawakilishi wa serikali ya mpito ya Somalia walioko Nairobi. |
Clinton azungumza na viongozi wa Kenya
Posted by
RAMADHANI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 maoni:
Post a Comment