Mashabiki wa nyota wa muziki wa Kizazi kipya Bongo Junior wamemtupia
zigo la lawama bosi huyo wa lebo ya sharobaro kwa kuwalaghai na
kushindwa kutimiza ahadi kumwonyesha mke wake mtarajiwa wakati wa shoo
yake aliyofanya ndani ya ukumbi wa Club Bilicannas jijini Dar.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Teentz.com mashabiki hao
wlaiojitambulisha kuwa ni wakazi wa Gongo la Mboto walisema kuwa
wameshindwa kumuelewa Bob Junior kwa kushindwa kuwaonyesha shemeji yao
na kisha kukaa kimya bila kusema lolote tangu kufanyika kwa shoo hiyo
jumapili iliyopita. "Binafsi sikupendezwa na hali hile kwani licha ya kuja kuburudika, nia yangu kubwa ilikuwa ni kumuona mkewa wa Bob Junior msanii ambaye kwangu mimi ninamkubari kuliko wengine wote waliopo kwenye game" alisema mmoja wa mashabiki hao aliyejitambulisha kwa jina la Mudi. Akiendelea zaidi Mudi alilalamika kuwa inavyoonekana ni kama Bob aliamua kuwadanganya watu juu ya jambo hilo ili apate watu wengi kwenye Shoo yake. Hata hivyo mpaka habari hii inakwenda hewani jubudi za Teentz .com kumsaka Bob ili azungumze kuhusiana na tuhuma hizi hazijafanikiwa |
BOB JUNIOR ATUPIWA ZIGO LA LAWAMA
Posted by
RAMADHANI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 maoni:
Post a Comment