WELCOME TO THE REPUTABLE BLOG IN TOWN WITH FANTASTIC NEWS,GOSSIP,TALENTS,FASHION,MOVIE STAY ON THIS WEBSITE
RSS

Polisi Ufaransa wamemzuilia mshukiwa

Eeneo anakoishi mshukiwa wa mauaji Ufaransa
Majususi wa Ufaransa wamemkamata mtu wanayeamini kuwa mshukiwa wa mauaji ya watu wanne wakiwemo, watoto watatu wa kiyahudi na mwalimu wao.
Mshukiwa huyo pia anaaminika kuwaua wanajeshi watatu.
Kwa mujibu wa kituo cha televisheni BFM, wametoa tangazo kumtaja mshukiwa huyo wakisema kuwa amezuiliwa ndani ya jengo lenye nyumba nyingi ambalo walilizingira tangu ashubuhi ya leo.
Muhammed Merah, ana umri wa miaka ishirini na nne, raia wa Algeria
Wakati mmoja mshukiwa huyo alitupa nje bunduki moja ingawa waziri wa mambo ya ndani Claude Gueant, anasema mtu huyo angali amejihami vikali.
Bwana Merah alizungumza na polisi wanaomshawishi mtu huyo kujisalimisha lakini baadaye akaodnoka kwenye eneo hilo.
Watu wengine wanaoishi katika jengo hilo wamehamishwa.

  • Digg
  • Del.icio.us
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • RSS

0 maoni: