Wakuu wa Syria wanasema miripuko miwili mjini Damascus imeuwa askari wa usalama na raia.
Picha za televisheni zilionesha viungo vya miili, damu na magari na majengo yaliyovunjika.
Wakuu wamewalaumu magaidi kwa mashambulio hayo, na wadadisi kwenye televisheni walizilaumu Saudi Arabia na Qatar, ambazo zinaunga mkono upinzani.
Hakuna aliyedai kuhusika na miripuko hiyo.
Wanaharakati wa upinzani siku za nyuma wameishutumu serikali kufanya mashambulio kama hayo ili kuonyesha kuwa inapigana na magaidi.
0 maoni:
Post a Comment