7 Februari, 2012 - Saa 02:32 GMT
Msimamo wa Urusi kuhusu matukio nchini Syria umeghadhabisha sana baadhi ya serikali za kimagharibi.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa Marekani Hilary
Clinton pamoja na chancellor wa ujerumani Angela Markel wameshutumu
hatua ya Urusi na China ya kupiga kura ya turufu kupinga azimio la
kuikosoa Syria katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Hatua hii ya Urusi itakuwa njia moja ya
kuonyesha kwamba kuna njia nyingine ya kukabiliana na kusitisha mapigano
yanayozidi kuongezeka nchini Syria.
Waziri wa masuala ya nje wa Urusi Sergei Lavrov
hata hivyo hajabainisha wazi nini maazimio yake atakapokutana na rais
Assad mjini Damascus akisema tu kwamba ametumwa na rais wake.
Hata hivyo ameelezea wazi msimamo wa Urusi
akisema ni raia wa Syria wala sio jumuiya ya kimataifa ndio wana uwezo
wa kuamua ni nani atakayekuwa rais wao.
0 maoni:
Post a Comment